Lyrics

Nilikuwa na rafiki yangu Rafiki Pesa Tulipendana sana Maisha yetu yalikuwa mazuri Nitakacho hunipatia Nilikuwa na rafiki yangu Rafiki pesa Tulipendana sana Maisha yetu yalikuwa mazuri Nitakacho hunipatia Nikitaka nyumba nzuri alikuwa anijengea Nikitaka gari nzuri alikuwa aniletea Nikitaka nguo nzuri anakimbia dukani aniletea Nikitaka suti nzuri alikuwa aniletea Nikitaka wanawake anakimbia Florida aniletea Nikitaka kunywa beer alikuwa aniletea (Instruments) Siku moja nilishikwa na ugonjwa mbaya sana Nikapelekwa kwa madakitari ugonjwa huo haukupona Waliposhindwa nikarudishwa nchini kwetu nyumbani kwangu Nikalazwa kitandani kwangu Nilikuwa naumwa sana Siku moja Rafiki Pesa akaja kwangu kunitazama Akaniambia Rafiki yangu pole sana kwa ugonjwa Usijali hata ukifa nitakununulia coffin Siku ile nilikufa Rafiki Pesa alitoroka Watoto wangu waliteseka Majirani waliwacheka Pesa alithamini, sasa maisha kwisha Utaenda wapi? Utaenda motoni Wakati urafiki wako na bwana Pesa unapoisha Mambo mawili anakufanyia Anakununua kitamba cheupe na coffin ya kukuingiza ndani (Instruments continues) Walevi walikunywa pombe wakashindwa na kutembea Wakitazama chini waona kuna mashimo Wavuta bangi walivuta sana Moshi nao ulipoganda Hata nywele za vichwa zao wakashindwa kuzichana Matajiri walipata pesa wakazieka kwa anasa Nazo pesa zaendelea kuwanunulia sanduku Matajiri walipata pesa wakazieka kwa anasa Nazo pesa zaendelea kuwanunulia jeneza (Instruments) Usithamini pesa Pesa zina mwisho, zina mwisho Pesa zina mwisho Raha nazo baba Raha zina mwisho, zina mwisho Raha zina mwisho Shika Yesu baba Yesu ndiye mwisho, ndiye mwisho Yesu ndiye mwisho Kwa wokovu Baba Yesu ndiye mwisho, ndiye mwisho Yesu ndiye mwisho Kwa wokovu Baba Yesu ndiye mwisho, ndiye mwisho Yesu ndiye mwisho
Lyrics powered by www.musixmatch.com
instagramSharePathic_arrow_out