Credits
PERFORMING ARTISTS
Nacha
Performer
COMPOSITION & LYRICS
Salum Othman Rashid
Songwriter
Lyrics
Killi.
Beaaa...
Mmh! Hebu ngojeni kwanza acheni kucheza bao
Tufanye huu mdahalo kuhusu mambo kibao
Hivi kwani ndo ujanja siasa za majitaka
Kwenye majukwaa
Kuvua na nguo na kupaka
Au ndo dalili ya ukomavu wa siasa
Aaah! aah! Nchi huru hii unafanya bwana unachotaka
Enhe Juma unasemaje eti una nini hapa?
Hizo ni njaa na ni tamaa za paka
Ajali barabarani chanzo chake ni nini?
Uzembe wa madereva na vitu vingi kichwani
Kwani matrafiki hawapo? mmh! Rushwa ni kufuru
Ah mbona siwaelewi? kwani haipo Takukuru?
Mfumo wa vyama vingi aloleta Nyerere
Mnauona unafanya kazi? Mmmh ni paka kengele
Hivi tutafuzu kombe la dunia kisha tunywe mvinyo?
Nyie Wabongo msahau hata kocha awe Mourinho
Kwa hio na mimi nikitaka madaraka naweza pata?(Eeeh... eeeh)
Alafu nikipata nitanata na simu nitakata(Aaah weee)
Mnaona vipi tukiishi bila udini matabaka(Eeeh... eeeh)
Hivi ni ungwana nikioa alafu kipigo talaka?(Aah aah weee)
Serikali ni watu na watu ndio sisi
Kwa hio nautamani urafiki wa raia na polisi
Mimba za utotoni? Nini unahisi?
Tatizo na watoto wanaponzwa sana na chipsi
Kama ni kweli basi hali inatisha
Nyie mnauona muungano wa zenji na Tanganyika?
Eeeh mbona bado upo hauoni Yanga Africa
Mo bacca Fei Makame bado anatisha
Hivi nilikuwa na wazo utani sesha swedi
Madada poa waruhusiwe ila walipe kodi
Alafu pesa zikasaidie wamama wodi
Hahaha hizo akili za ki odi
Mmmh dah, aisee wewe kwa hiyo walimu na madoctor
Nani mshahara waongezewe?
Mmmh bora walimu ila madoctor nao wenyewe
Aaah! hii Nchi ishauzwa nipeni mimi nikalewe
Kwa hio na mimi nikitaka madaraka naweza pata?(Eeeh... eeeh)
Alafu nikipata nitanata na simu nitakata(Aaah weee)
Mnaona vipi tukiishi bila udini matabaka(Eeeh... eeeh)
Hivi ni ungwana nikioa alafu kipigo talaka?(Aah aah weee)
Ni sawa Simba na Yanga vilabu kongwe vya soccer
Kumilikiwa na mtu mmoja kama Mo anavyotaka
Itapandisha soccer au mfumo itaporomosha
Hio ni vita kubwa kuna watu riziki watakosa muraa
Kwa mfano sasa, shule za kata ni ongezeko ufaulu
Ama bado zero NECTA
Faulu kivipi? Wanafunzi mia sita
Alafu walimu watano acheni kujifurahisha
Haya si walimtukana mzee juzi walilia ka watoto
Hee si walimtukana mamba kabla hawajavuka mto?
Tena na hili linanichanganya kuhusu sisi vijana
Maambukizi ya zinaa na mipira mingi sana
Tunazidi kuungua sababu ya uzembe sana
Aah soksi za nini na tumezaliwa peku
Kwaiyo Mchungaji kula kondoo hio ni sawa bila wasi
Hata Fisi akikosa nyama huwanga anakula nyasi
Kwa hio na mimi nikitaka madaraka naweza pata?(Eeeh... eeeh)
Alafu nikipata nitanata na simu nitakata(Aaah weee)
Mnaona vipi tukiishi bila udini matabaka(Eeeh... eeeh)
Hivi ni ungwana nikioa alafu kipigo talaka?(Aah aah weee)
Nyasubi nda Nyambano beiby
Wamemchokoza bea...
Lyrics powered by www.musixmatch.com