Lyrics

Merimela kipenzi rafiki wa karibu tangu hapo zamani Tulipoanza shule nasi tukiwa watoto ulikuwa mpole Tena mwenye adabu msichana mrembo kila mara mshindi Sifa nazo urembo ukaenea kwote ukipita ni whispers Wa darasa la saba kipenzi Merimela ukaanza geuka Machali mbalimbali ata nao walimu wakakufanya quencher Na wewe ukakubali ingilia mapenzi ya kiholelaholela Na we kuwashukia waliokuwa karibu wakukupa ushauri Nami nikakuonya, chunga sana maisha Na we kashauriwa, badilisha mienendo Na we ukapuuza, waenjoy maisha Tena ukakataa, unavunja mifupa Ukakosa bahati mrembo Merimela ukakwachua mimba Ukazunguka kwote ukitaka mawaidha juu ya mimba mpenzi Nawe ukadanganywa toa kitu kidogo ukafanya abortion Bila kushauriwa njia gani salama ya kujilinda mrembo Ukaambiwa uchili, ukasema ni ndoto Utumie mipira, ukasema si tamu Basi panga uzazi, ukasema ni hectic Heri upate wokovu, ukakataa ni mapema Kwa shule ya upili mwendo ni ule ule mapenzi kiholela Kila mwaka ni mimba, kila mwaka abortion, ikakuwa mtindo Ata chuo kikuu raha ikapanda, vunjavunja mifupa Wadosi na fukara ukaonja Merimela na mimba ni kawaida Ukakuwa ni dustbin, ya kutupa takataka ATM mashini, kila kadi yaingia Ukakuwa daladala, kila mtu akupanda Bado nakumbuka siku ulionialika kwa harusi Merimela Ukanielezea umekwisha hitimu na umepata mchumba Kama rafiki yako kanisisitizia nisikose kufika Kazi umeshapata na mshahara unapata na itakuwa sherehe Mimi kama rafiki, nikafika huko mapema Ilikuwa ni sherehe [kubwa sana], ya vifijo na nderemo Nilikuwa ni maombi [Haleluyah], na zawadi teletele Kila uso ni furaha [hahaha], siku hiyo ya harusi Sasa miaka mitano imepita Merimela hujapata mtoto Kila siku kelele kati yako na bwana, anataka mtoto Ata na wakwe zako wanapiga kelele, wanataka mtoto Furaha imekwisha imebaki huzuni, kila siku mawazo Kwa waganga umeenda, hujapata mtoto Kwa maombi umeenda, hujapata mtoto Dakitari akasema, beba mimba huwezi Dakitari akasema, beba mimba huwezi Na uchungu ya machungu umepatwa na virusi Na uchungu ya machungu umepatwa na virusi Mela mama Usilie usilie Mela mama, usilie Mela mama Usilie Mela mama, usilie Mela mama Unanafasi ya kuishi usilie, Fanya tizi, fanya tizi eh
Lyrics powered by www.musixmatch.com
instagramSharePathic_arrow_out